Wednesday, January 7, 2015

Na Amplifaya Amplifaya

NILICHOJIFUNZA na kukigundua kuhusu sisi mashabiki wa Tz kiukweli huwa hatuna uvumilivu na tunapenda mafanikio ya hapo kwa papo. Hatunaga subira.

Tumekuwa tukihukumu wachezaji wengi hasa wale wanaotoka nje ya nchi kuja nchini kwetu kucheza soka.

Tunataka wakija Leo wang'ae Leo Leo .Tunasahau kuna vitu vingi vinaweza kumsababisha mchezaji kushindwa kung'ara ikiwemo kubadilisha mfumo aliouzoea.

Jinsi anavyocheza, je ni mchezaji gani alikuwa anamchezesha kwenye timu aliyotoka na wakati huku alipo sasa hakuna mtu wa aina ile.
Pia ugumu wa ligi, hali ya hewa na mengi kama hayo.


Hivyo mchezaji kama huyu anatakiwa kupewa muda kuzoea mazingira, mfumo pamoja na wachezaji aliowakuta.

Yanga chini ya Maximo, Coutihno na wenzake walionekana si chochote kutokana na mfumo mgumu wa kocha huyo.

Jaribu kumtazama Coutihno wa sasa chini ya mfumo wa Hans van der Pluijm

Upande wa Simba nao kuna baadhi ya watu wanamtupia lawama Danny_Serunkuma kitu ambacho sio sahihi maana mchezaji mwenyewe hana hata miezi sita kuichezea Simba.

Ni wachezaji wangapi walikuja TANZANIA tukawaona magarasa tukawatimua na wakarudi makwao wakapata timu zakuchezea na wakang'ara na wakaja kutuhukumu pale pale kunako dimba la taifa?


Mpira hapa bongo kwetu unaongozwa na wasanii watupu.
Huku wataalamu hawa hawa wachache tulionao wakipigwa mawe na kudharauliwa.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video