Kocha mkuu wa Simba, Goran Kopunovic akiwa amewahi kupanga viti vya benchi la Simba kwenye moja ya mechi ya kombe la Mapinduzi zinazoendelea hapa Zanzibar
OJA ya vitu anavyopenda kocha mpya wa Simba,
Goran Kopunovic ni kuzingatia muda, nidhamu, kujituma na heshima.
Wachezaji wengi wa kitanzania wamekuwa na matatizo
katika mambo hayo anayopenda kocha huyo raia wa Serbia hasa kutozingatia muda.
Kopunovic katika programu zake za mazoezi hataki
hata kupoteza dakika moja.
Meneja wa Simba, Nico Nyagawa amekiri kuwepo kwa
mabadiliko katika kikosi chao hasa suala la muda.
“Ni kocha anayezingatia sana muda, hataki kupoteza
hata dakika moja. Hili ni jambo muhimu sana kwasababu wachezaji wengi wa
Kitanzania wana tatizo la kutofuata muda”. Alisema Nyagawa.
0 comments:
Post a Comment