THEO Walcott alifurahia
kurudi uwanjani katika ushindi wa 2-0
iliopata Arsenal kwenye mechi ya raundi ya tatu ya FA jana jumapili na ameeleza furaha yake kucheza na mchezaji
maalum, Alexis Sanchez.
Walcott alicheza dakika 76 dhidi ya Hull City uwanja wa Emirates
na amefurahia kucheza mechi ya kwanza baada ya mwaka kupita tangu alipopata
majeraha ya goti na alikosa fainali za kombe la dunia mwaka jana.
“Alexis Sanchez ni mchezaji maalumu na imekuwa furaha kucheza
naye uwanjani. Naangalia mbele kufanya makubwa zaidi”, Alisema Walcott.
0 comments:
Post a Comment