LIGI kuu Tanzania bara imeendelea leo kwa mechi
kadhaa kupigwa viwanja mbalimbali nchini.
Huko CCM Mkwakwani Tanga, JKT Ruvu wamefanikiwa
kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya wenyeji Coastal Union ya Tanga.
Bao pekee la JKT Ruvu lilifungwa na Samuel Kamuntu
katika dakika ya 38.
Maafande wa Polisi Morogoro wakiwa uwanja wa
nyumbani wa Jamhuri Morogoro wametoka suluhu pacha ya bila kufungana dhidi ya
Stand United ya Shinyanga.
Ruvu Shootings ikuwa nyumbani Matabatini,
Mlandizi, Pwani imelazimishwa suluhu ya bila kufungana na Kagera Sugar ya
Mkoani Kagera.
0 comments:
Post a Comment