Tuesday, January 27, 2015


Na Bertha Lumala, Dar es Salaam 
LIGI Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) iliingia raundi ya 12 wikiendi iliyopita huku mshambuliaji Samwel Kamuntu akionesha kuwa amepania kukinyakua kiatu cha mfungaji bora baada ya kufunga katika mechi nne mfululizo.

Kamuntu amekuwa lulu katika kikosi cha kocha mzawa Fred Felix Minziro cha JKT Ruvu Stars ambacho sasa kinakamata nafasi ya tatu kikiwa na pointi 18 sawa na Yanga SC walioko nafasi ya pili kwa faida ya tofauti nzuri ya mabao ya kufunga na kufunga, pointi tatu nyuma ya vinara Azam FC.

Mshambuliaji huyo alifunga bao lake la tano msimu huu juzi katika mechi yao ya jana waliyotoka sare ya 1-1 dhidi ya Mgambo Shooting Stars Uwanja wa Azam, Dar es Salaam.

Kamuntu alifunga pia katika mechi zote nne zilizopita dhidi ya Coastal Union FC, Stand United FC, Mtibwa Sugar FC na ya juzi dhidi ya kikosi cha Bakari Shime cha Mgambo. 

Byota huyo sasa ana mabao matano sawa na Ame Ally Amour wa Mtibwa Sugar FC, Rashid Mandawa wa Kagera Sugar FC na Danny Mrwanda wa Yanga SC.
     
WAKALI WA KUCHEKA NA NYAVU VPL
7. Didier Kavumbagu   Azam FC            
------------------------------------------------------------------
5. Ame Ally Amour      Mtibwa Sugar 
Rashid Mandawa        Kagera Sugar    
Danny Mrwanda         Polisi/Yanga SC 
Samwel Kamuntu       JKT Ruvu Stars  
-----------------------------------------------------------------
4. Rama Salim            Coastal Union   
Simon Msuva              Yanga SC            
Emmanuel Okwi          Simba SC           
------------------------------------------------------------------
3. Ally Shomary Sharif  Mtibwa Sugar   
Nassoro Kapama          Ndanda FC
Kipre Tchetche             Azam FC
-----------------------------------------------------------------
2. Aggrey Morris          Azam FC            
Amisi Tambwe             Simba/Yanga SC
Deus Kaseke               Mbeya City FC
Ibrahim Hassan           Tanzania Prisons
Jabir Aziz                     JKT Ruvu Stars
Jacob Masawe             Ndanda FC
Mussa Mgosi                Mtibwa Sugar FC
Najim Magulu               JKT Ruvu Stars
Nicholas Kabipe           Polisi Moro
Shaban Kisiga              Simba SC 
---------------------------------------------------------

TANO ZA JUU
Na.Timu    Pld    W     T     L    GF GD Pts
1.  Azam    11      6     3     2     15    7   21
2.  Yanga   10     5     3     2     12    4   18
3.  JKT       12     5     3     4     12    1   18
4.  Mtibwa  10     4     5     1     13    6   17
5   Coastal 11     4     4     3     10    2   16

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video