Sunday, January 18, 2015

LIGI kuu Tanzania bara inaendelea kwa mechi mbili kupigwa viwanja viwili tofauti nchini.

Wagosi wa Kaya waliofanya maandalizi makubwa wakicheza mechi ya kirafiki na Kombaini ya Mombasa mwishoni mwa wiki iliyopita na kutoka sare ya 1-1 kwa lenngo la kupata makali wanachuana vikali na Polisi Morogoro.

Mechi hiyo kali inapigwa uwanja wa CCM Mkwakwani Tanga ambapo mashabiki wa Coastal wataingia kuona namna kikosi chao kilivyobadilika.

Mabingwa hao wa Tanzania mwaka 1988 wanaonekana kuwa na ubora msimu huu tofauti na mwaka jana, lakini Wapinzani wao Polisi Moro wanaonolewa na Adolf Rishard nao wamekuwa wapinzani wa kweli.

Mechi nyingine itapigwa katika uwanja wa Azam Complex ambapo vinara wa ligi kuu, Mtibwa Sugar watakabiliana na wenyeji JKT Ruvu.

Mtibwa Sugar ambao hawajafungwa mechi yoyote mpaka sasa wanaingia na machungu ya kutandikwa na Simba penalti 4-3 na kupokwa kombe la Mapinduzi.

Mechi hiyo ya fainali ilichezwa januari 13 mwaka huu uwanja wa Amaan Kisiwani Unguja Zanzibar.

Ligi kuu iliendelea jana kwa mechi tano kupigwa na matokeo yako kama ifuatavyo:

Yanga SC v Ruvu Shootings

0 :0


Kagera Sugar FC v Mbeya City FC


0 : 1


Ndanda fc v Simba sc


0 : 2


Stand United v Azam fc


0: 1


Mgambo JKT v Tanzania Prisons


0 : 0



0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video