Saturday, January 17, 2015

KOCHA mkuu wa Simba SC, Goran Kopunovic yuko tayari kuiongoza timu yake katika mchezo wake wa kwanza wa ligi kuu soka Tanzania bara utakaopigwa uwanja wa CCM Nangwanda Sijaona jioni ya leo Mkoani Mtwara.
Kwa mujibu wa Afisa habari wa Simba, Humphrey Nyasio ambaye amezungumza na mtandao huu asubuhi hii kwa njia ya simu kutoka Mtwara, Kikosi cha Simba hakina majeruhi yeyote na kocha amefurahishwa na hali hiyo.

“Tuko ‘fresh’ kabisa. Jana jioni tulifanya mazoezi na mashabiki wengi walijitokeza kutuona mabingwa wa kombe la Mapinduzi. Hii inaashiria wanaiamini timu yao.” Amesema Humphrey. “Kocha amekiandaa kikosi chake na ameeleza kuwa yuko tayari kwa ajili ya mechi”.

Kopunovic anapenda soka wa wazi la kumiliki mpira, kushambulia kwa kasi na kukaba kwa umakini kuanzia safu ya kiungo na kipindi ambacho ameiongeza Simba kombe la Mapinduzi, vijana wameonekana kuwa na mabadiliko kiuchezaji.

Tusubiri kuona Mserbia huyu atavuna nini katika mechi ya ligi na ikumbukwe kwamba Simba hawaja na matokeo mazuri mpaka sasa.


Katika mechi nane walizocheza, wametoka sare mechi sita, wamefungwa moja na kushinda moja.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video