Wachezaji wa Yanga wakifanya mazoezi leo uwanja wa Boko Veteran
YANGA itawakosa Mbuyu Twite na Nadir Haroub
‘Cannavaro’ katika mechi ya kesho ya ligi kuu soka Tanzania bara itakayopigwa
uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam dhidi ya Ruvu Shootings.
Twite ana majeruhi ya goti aliyopata katika
mazoezi ya timu hiyo katikati ya wiki hii, wakati Cannavaro anamalizia adhabu
yake ya kufungiwa mechi tatu.
Licha ya kuwakosa wachezaji hao muhimu wa kikosi
cha kwanza, kocha mkuu wa Yanga, Mholanzi, Johannes Hans van der Pluijm amesema
wana matarajio makubwa ya kupata ushindi kwani kwa wiki nzima wamefanya mazoezi
ya ufundi.
Moto ukiwa umekolea katika mazoezi ya Yanga leo
Akizungumza katika mazoezi ya Yanga yaliyofanyika
leo uwanja wa Boko Veteran, Pluijm anayependa mpira wa wazi na kushambulia kwa
kasi amesema nafasi ya mabeki wa kati atawaanzisha Rajab Zahir na Kelvin
Patrick Yondani.
0 comments:
Post a Comment