Thursday, January 8, 2015

Toure eyes record; history beckons Aubameyang, Enyeama
UKURASA mpya utaandikwa katika historia ya soka la Afrika pale atakapopatikana mchezaji bora wa Afrika kwa mwaka 2014.

Kuna historia inayowazunguka wachezaji watatu wanaopewa nafasi kubwa ya kutwaa tuzo hiyo; mshambulaiji wa Gabon, Pierre-Emerick Aubameyang, golikipa wa Nigeria Vicent Enyeama na kiungo wa Ivory Coast Yaya Toure.

Wachezaji hao watatu wote walikuwa na msimu mzuri katika timu zao za taifa na klabu zao na kuwafanya wakaribiane zaidi kutwaa tuzo hiyo. Kila mmoja anastahili kupewa tuzo ya Mwanasoka bora wa Afrika.

Toure, mshindi wa tuzo hiyo mara tatu mfululizo anakabiliana na upinzani mkubwa kutoka kwa Aubameyang na Enyeama katika harakati zake za kutaka kutwaa tuzo hiyo kwa mara nne mfululizo.

Nyota wa zamani wa Cameroon, Samuel Eto’o ndiye mchezaji pekee aliyeshinda tuzo hiyo mara nne -mwaka 2003, 2004, 2005 na 2010.

Toure ndiye mchezaji anayetaka kuifikia rekodi hiyo ya Eto’o, lakini pia anahitaji kuwa mchezaji pekee aliyetwaa tuzo za mwanasoka bora wa Afrika mara nne mfululizo.

Aubameyang na Enyeama pia wana rekodi zao walizoweka. Nyota huyo wa Gabon atakuwa mchezaji wa kwanza wan chi hiyo kutwaa tuzo hiyo ya heshima tangu mwaka 1992.

Kama Enyeama atashinda  tuzo hiyo atakuwa golikipa wa kwanza kufanya hivyo. Pia atakuwa Mnigeria wa kwanza kutwaa tuzo hiyo tangu mwaka 1999.

Mshambuliaji Gwiji wa Nigeria, Nwankwo Kanu ndiye alikuwa Mnigeria wa mwisho kutwaa tuzo hiyo mwaka 1999. Wanigeria wengine walioshinda tuzo hiyo ni Rashidi Yekini (1993), Emmanuel Amunike (1994) na Victor Ikpeba (1997).

Enyeama

Kwa upande wa mchezaji bora wa Afrika anayecheza soka la ndani, waalgeria wawili, Akram Djahnit na El Hedi Belamieri  watapambana na mshambuliaji wa DR Congo, Firmin Mubele Ndombe. Mshindi atapatikana kwa kura zitakazopigwa na Makocha wakuu au wakurugenzi wa ufundi wa vyama wanachama wa CAF.

Shoo hiyo ya kumpata mwanasoka bora wa Afrika itafanyika kwa dakika 180 na sherehe hizo zitatumbuizwa na wanasanii wakubwa wa Afrika. 

Mapacha wawili wa Hip Hop, P-Square watatoa burudani kali mbele ya umati wa watu watakaohudhuria sherehe hizo.

 Pia Lagbaja atatumbuiza sambamba na wasanii wengine kama vile Fally Ipupa; global Jazz icon, Hugh Masekela  kutoka Afrika kusini, mwimbija wa Misri, Hakim.

 Wasanii wengine ambao watatumbuiza katika shoo hiyo itakayooneshwa moja kwa moja duniani kote watakuwa ni  Soweto Gospel Choir  kutoka Africa kusini, kundi la kwaya la Uhuru; pan African group, Cirque D’Afrique na nyota wa muziki Tanzania, Diamond Platinumz.


HAPA CHINI NI ORODHA YA TUZO MBALIMBALI ZINAZOWANIA BARANI AFRIKA


MCHEZAJI BORA WA AFRIKA (wamepangwa kwa kufuata alphabeti)

Pierre-Emerick Aubameyang (Gabon na Borussia Dortmund)

Vincent Enyeama (Nigeria na Lille)

Yaya Toure (Cote d’Ivoire na  Manchester City)


MCHEZAJI BORA WA AFRIKA-Anayecheza soka Afrika

Akram Djahnit (Algeria na ES Setif)

El Hedi Belamieri (Algeria  na ES Setif)

Firmin Mubele Ndombe (DR Congo na AS Vita)


MCHEZAJI BORA WA AFRIKA WANAWAKE

Annette Ngo Ndom (Cameroon na Amazon Grimstad)

Asisat Oshoala (Nigeria na River Angels)

Desire Oparanozie (Nigeria na Guingamp)


MCHEZAJI BORA AFRIKA KIJANA

Asisat Oshoala (Nigeria na River Angels)

Fabrice Ondoa (Cameroon na Barcelona)

Uchechi Sunday (Nigeria na River Angels)


MCHEZAJI BORA ANAYECHIPUKIA

Clinton N’jie (Cameroon na Olympique Lyon)

Vincent Aboubakar (Cameroon na Porto)

Yacine Brahimi (Algeria na Porto)


KOCHA BORA WA MWAKA

Florent Ibenge (DR Congo)

Kheireddine Madoui (ES Setif)

Vahid Halilhodžić (Kocha wa zamani wa Algeria)


TIMU BORA YA TAIFA YA MWAKA 2014

Algeria

Libya

Nigeria


TIMU BORA YA TAIFA YA WANAWAKE YA MWAKA

Cameroon

Nigeria

Nigeria U-20


KLABU BORA YA MWAKA

Al Ahly (Egypt)  

AS Vita (DR Congo)

Sewe Sport (Cote d’Ivoire)


MWAMUZI BORA WA MWAKA

Alioum Neant (Cameroon)

Doue Noumandiez Desire (Cote d’Ivoire)

Papa Bakary Gassama (Gambia)


KIONGOZI BORA WA MPIRA WA MWAKA

Moise Katumbi Chapwe – Rais wa TP Mazembe (DR Congo)


TUZO YA GWIJI WA AFRIKA

Oryx Club (Cameroon) – winners of the maiden edition of CAF Champions League 1964


Stade Malien (Mali) - runner up of the maiden edition of CAF Champion’s League 1964

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video