NYOTA aliyekulia Atletico Madrid na
sasa amerejea tena Fernando Torres leo jumatano anaweza kucheza mechi yake ya
kwanza dhidi ya mahasimu wa jadi Real Madrid, mechi ya hatua ya 16 ya Kombe la
Mfalme.
Katika mazoezi ya jana, kocha mkuu wa
Atletico Diego Simeone alisema Torres alionekana kushika mbinu kwa haraka.
Nahodha huyo wa zamani wa Real Madrid
ambaye alicheza mehi 244 klabuni hapo akiwa na miaka 17 alisaini mkataba wa
miezi 18 kwa mkopo kutoka AC Milan na utaanza kutumika mara baada ya dirisha la
usajili ulaya kufunguliwa jumatatu ijayo.
0 comments:
Post a Comment