Saido Berahino hazingatii muda
KUTOZINGIA muda ni moja ya matatizo yanayomkabili mshambuliaji msumbufu wa West Brom, Saido Berahino, ambaye hakushangilia hata goli moja kati ya magoli manne aliyofunga katika ushindi wao wa mabao 7-0 dhidi ya Gateshead kombe la FA..
Berahino ameripotiwa kuchelewa mara tatu siku za mechi msimu huu, na hivi karibuni alichelewa katika mechi ya timu yake dhidi ya Manchester City, siku ya 'Boxing Day' ambapo alilipa faini.
Mshambuliaji huyo mwenye asili ya Burundi ambaye aliitwa katika kikosi cha England kwa mara ya kwanza dhidi ya Slovenia ingawa hakuceza, alikamatwa kwa kosa la kuendesha gari akiwa amelewa mwezi oktoba mwaka jana na kusababisha West Bron iahirishe mazungumzo ya mkataba wake mpya.
Kwa sasa kiwango cha nyota huyo kimeshuka kwa haraka mpaka jumamosi iliyopita.
Kocha mpya, Tony Pulis anatarajiwa kuinua kiwango cha nyota huyo mwenye maiaka 21 kuliko kumuuza mwezi huu licha ya Liverpool kuonesha nia.
0 comments:
Post a Comment