MGANDA Simon Sserunkuma na Mzawa Said Hamis Ndemla
wapo tayari kuivaa Ndanda fc katika mechi ya kesho ya ligi kuu soka Tanzania
bara itakayopigwa uwanja wa Nangwanda Sijaona.
Afisa habari wa Simba, Humphrey Nyasio ameuambia
mtandao huu dakika chache zilizopita kuwa Simon aliyeumia kwenye mechi ya nusu
fainali ya kombe la Mapinduzi dhidi ya Polisi na kuukosa mchezo wa fainali na
Mtibwa Sugar ambapo Simba ilishinda kwa penalti 4-3 na kutwaa kombe jana
alifanya mazoezi kwa asilimia 100.
Pia Ndemla aliyeumia kwenye mechi ya fainali ya
Mapinduzi januari 13 mwaka huu yuko kamili gado kuwavaa Ndanda wenye usongo wa
kupata pointi tatu muhimu.
“Wachezaji wote wazima, Simon na Ndemla wako safi
kabisa, hakuna tatizo. Jana tumefanya mazoezi na leo jioni tunaenda kufanya
mazoezi ya mwisho kabla ya mechi ya kesho”. Alisema Nyasio.
Kikosi cha Ndanda fc
Simba wenye morali kubwa baada ya kutwaa taji la
Mapinduzi wataingia uwanjani wakiwa na kumbukumbu ya kufungwa bao 1-0 na Kagera
Sugar desemba 26 mwaka jana na kipigo hicho kilimfukuzisha kazi kocha mkuu
Patrick Phiri.
Kocha mpya Goran Kopunovic baada ya kufanya kazi
nzuri Zanzibar ataiongoza Simba kwa mara ya kwanza katika mechi ya ligi kuu.
Katika
mechi 8 za kwanza, Simba ilitoa sare sita, ikashinda moja na kufungwa moja.
0 comments:
Post a Comment