KOCHA mpya wa Simba, Goran Kopunovic ameanza vyema
kibarua chake Msimbazi baada ya jioni ya leo kuiongoza klabu yake kuibuka na
ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Mafunzo ya Zanzibar katika mchezo wa kundi C kombe
la Mapinduzi 2015.
Bao pekee la Mnyama lilitiwa kambani dakika ya 55
kipindi cha pili kupitia nyota mwenye kipaji cha hali ya juu, Said Hamis
Ndemla.
Ndemla alitia gozi kambani kwa shuti kali nje ya 18 kufuatia
pasi murua aliyotengenewa na beki wa kulia Hassan Ramadhani Kessy.
Ushindi huo ni faraja kwa mashabiki na wapenzi wa
Simba kwani mechi ya kwanza walitandikwa 1-0 na Mtibwa Sugar fc.
Katika mchezo wa leo, Makamu wa Rais wa Simba,
Geofrey Nyange Kaburu alihuduhuria na kukunwa na matokeo waliyopata.
Kocha Mkuu wa Simba, Goran Kopunovic
Hata hivyo, kocha Goran alionekana kutoridhishwa na
kiwango cha timu na alitumia muda mwingi kuwaelekeza wachezaji wake nini cha
kufanya.
Kocha Goran aliwaanzisha Hassan Kessy, Mohamed
Hussein ‘Tshabala’, Hassan Isihaka na Abdi Banda katika safu ya ulinzi.
Kikosi cha Simba kilichoanza leo
Jonas Mkude alicheza kiungo wa ulinzi wakati winga
ya kulia alianza Ramadhan Singano ‘Messi’, winga ya kushoto Awadh Juma na
washambuliaji wa kati walianza Danny Sserunkuma na Elius Maguli.
Kikosi cha Mafunzo
Michuano hiyo itandelea kesho kwa mechi nne
kupigwa ambapo mabingwa watetezi KCC ya Uganda watachuana na Mtende katika
uwanja wa Amaan kuanzia majira ya saa 9:00 alasiri.
Mechi ya pili itaanza majira ya saa 11:00 katika
uwanja huo huo ambapo Yanga wataoneshana kazi na Polisi na baadaye usiku saa
2:00 Azam fc watapepetana na KMKM.
Mechi nyingine itapigwa katika uwanja wa Mao dze
Tung kwa kuwakutanisha Taifa ya Jang’ombe na Shaba.
0 comments:
Post a Comment