Friday, January 30, 2015


Ibrahim Hajib (katikati) alishindwa kuiokoa Simba na kipigo cha 2-1 kutoka kwa Mbeya City fc licha ya kufunga goli la kuongoza

MABINGWA wa kombe la Mapinduzi 2015, Simba SC kesho wanasaka pointi tatu kwa kila namna  ili kupunguza machungu waliyopata kwa kutandikwa mabao 2-1 dhidi ya Mbeya City katika mechi ya ligi kuu iliyopigwa juzi, januari 28 uwanja wa Taifa Dar es salaam.

Simba watavaana na Maafande wa JKT Ruvu Stars  wanaonolewa na kocha wa zamani wa Yanga, Fredy Minziro, katika mechi ya VPL itayopigwa uwanja wa Taifa, Dar es salaam.

Huu ni mtihani wa tatu kwa kocha wa Simba SC, Goran Kopunovic kwani tayari ameshaiongoza timu hiyo katika mechi mbili za ligi kuu.

Kopunovic alianza ligi kuu kwa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Ndanda fc, Januari 17 mwaka huu, kabla ya kulazimisha sare ya 1-1 na Azam fc, Januari 24 mwaka huu. Juzi wakalala 2-1 dhidi ya Mbeya City.

Tayari baadhi ya wanachama na mashabiki wa Simba wameanza chokochoko wakimtaka Rais wa Simba, Evans Aveva ajiuzulu kutokana na kushindwa kuweka umoja katika klabu hiyo.

Aveva ambaye haamini kama mgogoro wa Simba na wanachama wake wa UKAWA ndio chanzo cha kuboronga kwa timu, amekaririwa mara kadhaa kuwa uongozi wake hauko tayari na hauna mpango wa kukutana na kundi hilo maarufu nchini.

Lakini jana, Mwenyekiti wa kamati ya usajili wa Simba, Zacharia Hans Poppe ambaye alifungua milango kwa UKAWA kurudi klabuni kama watafuta kesi yao Mahakamani alisema wanasimba hawana haja ya kuwalaumu viongozi kwa matokeo mabaya.

“Mchezaji kukosa penalti (Masoud Nassor Cholo) unamlaumu vipi kiongozi. Labda yeye ndiye aulizwe amekosaje penalti”. Alikaririwa Hans Poppe akiwatetea viongozi kutohusika na matokeo hayo.

Hata hivyo alisema kuna haja ya kufanya uchunguzi ili kubaini kama kuna hujuma klabuni hapo.

Simba inakabiliwa na matokeo mabaya ambapo mpaka sasa wameshinda mechi mbili tu dhidi ya Ruvu Shootings na Ndanda fc katika mechi 11 walizocheza.

Wamefungwa mara mbili dhidi ya Kagera Sugar na Mbeya City na kutoka sare saba.

Tayari kocha Kopunovic ameshatoa kauli ya kuwakatisha tamaa Wanasimba kwamba wasahau kutwaa ubingwa mwaka huu.


Kocha huyo alisema kama Simba wanawaza Ubingwa basi nayeye atafukuzwa kama ilivyotokea kwa makocha wengine waliomtangulia kwani haamini kama ana kikosi cha Ubingwa.

Mpaka sasa Simba wapo nafasi ya 11 wakijikusanyia pointi 13 katika mechi 11 walizocheza.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video