Monday, January 19, 2015

Baada Ndanda fc sasa zamu ya Azam fc

WEKUNDU wa Msimbazi Simba wanaanza mazoezi kesho asubuhi kuitafutia dawa Azam fc wakayopambana nayo katika mechi ya ligi kuu soka Tanzania bara itayofanyika uwanja wa Taifa, Dar es salaam.
Meneja wa Simba, Nico Nyagawa ameuambia mtandao huu asubuhi hii kuwa kocha Goran Kopunovic  alitoa mapumziko kuanzia jana jioni na leo baada ya ushindi wa mabao 2-0 waliopata jumamosi iliyopita dhidi ya Ndanda fc kwenye uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mkoani Mtwara.

“Tunaanza mazoezi kesho asubuhi, lakini bado hatujathibitisha uwanja tutakaotumia, kufikia baadaye mchana nitatoa taarifa niwapi tutakuwa na program”. Amesema Nyagawa.


Mechi hiyo ya wikiendi itakuwa ya pili katika ligi kwa kocha Kopunovic ambaye mpaka sasa hajafungwa mechi yoyote tangu aanze kazi ya kuifundisha Simba katika michuano ya kombe la Mapinduzi na alifanikiwa kutwaa kombe hilo januari 13 mwaka huu kwa kuifunga Mtibwa Sugar penalti 4-3 katika mechi ya fainali.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video