Danny Sserunkuma alianzia benchi
WEKUNDU wa Msimbazi Simba wamechapwa bao 1-0 dhidi
ya Mtibwa Sugar katika mchezo wa kundi B wa kombe la Mapinduzi lililoanza
kutimua vumbi leo visiwani Zanzibar.
Bao pekee la ushindi kwa Mtibwa Sugar limefungwa
na kiungo wa zamani wa Simba na nahodha wa Taifa Stars, Henry Joseph Shindika katika
dakika ya 44 kipindi cha kwanza.
Katika mechi hiyo, wachezani wanne wa kigeni wa
Simba, Juuko Musheed, Joseph Owino, Simon Sserunkuma na Emmanuel Okwi
hawakuwepo kikosini.
Danny Sserunkuma pekee ndiye alikuwepo, hata hivyo
alianzia benchi na alipoingia alijitahidi kutafuta bao la kusawazisha, lakini
malengo yake yaligonga mwamba.
Wakati huo huo, Kocha mkuu mpya wa Simba sc, Goran
Kapunovic aliyesaini mkataba wa mwaka mmoja mchana wa leo alihudhuria mechi
hiyo iliyopigwa uwanja wa Amaan Unguja.
Mechi hiyo ilitanguliwa na mechi mbili ambapo JKU
waliitandika mabao 2-0 Mafunzo, zote za Zanzibar. Mechi ya pili Shaba
iliitandika baoa 1-0 Polisi.
0 comments:
Post a Comment