Kikosi kilekile kilichoanza dhidi ya JKU kinaanza leo
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar
MGANDA Saimon Sserunkuma ambaye hukuwepo katika
mechi tatu za makundi za kombe la Mapinduzi leo majira ya saa 2:15 usiku katika
uwanja wa Amaan Zanzibar mjini hapa anaanzia benchi Simba SC ikipepetana na
Taifa ya Jang’ombe kwenye kipute cha kwanza cha Robo fainali ya kombe hilo.
Kocha mkuu wa Simba, Mserbia Goran Kopunovic amemuanzisha
langoni Manyika Peter, wakati beki wa kulia anaanza Hassan Ramadhani Kessy na
Mohammed Hussein ‘Tshabalala’ anaanza mbavu ya kushoto.
Mabeki wa kati ni Juuko Mursheed na Hassan
Suleiman Isihaka.
Kiungo wa ulinzi anaaza Jonas Gerard Mkude , kiungo
namba nane anaanza Said Ndemla, wakati winga ya kulia anaanza mfungaji wa goli
lililoivusha Simba Robo fainali dhidi ya JKU, Ramadhani Singano ‘Messi’.
Winga ya kushoto ataanza Awadh Issa Juma na
mshambuliaji wa kati anasimama Elius Maguli na nyuma yake (kiungo mshambuliaji
namba 10) anaaza Danny Sserunkuma.
Wachezaji wa akiba ni Denis Richard, Nassor
Masoud, Issa Rashid, Abdallah Seseme, Ibrahim Ajib, Ibrahim Twaha, Shaban
Kisiga, Simon Sserunkuma na Abdi Banda.
Kopunovic ataanza na mfumo wa 4-2-2 ambao
unatumiwa zaidi na Mnyama Simba.
Kikosi cha
kwanza hakina mabadiliko, wachezaji wote walianza katika mechi ya mwisho ya
makundi Simba ikishinda bao 1-0 dhidi ya Vinara wa Zanzibar, JKU.
0 comments:
Post a Comment