Mshambuliaji wa Liverpool, Raheem Sterling
Liverpool wanajipanga kuwafurahisha mashabiki wao kwa kumuongeza mkataba mwingine Raheem Sterling kufikia mwishoni mwa mwezi huu.
Mkataba huo utaigharimu klabu hiyo ya Anfield paundi milioni 25.
Majogoo hao wa jiji wanamatumaini ya kumbakisha Sterling kwa mkataba wa miaka mitano ambapo atakuwa analipwa paundi laki moja kwa wiki na tayari mazungumzo baina ya pande mbili yameshaanza baada ya taarifa za kushangaza kwamba nahodha Steven Gerrard anaondoka kwenda kucheza soka Marekani.
0 comments:
Post a Comment