Saturday, January 24, 2015

Andrey Coutinho (kushoto) na Kpah Sherman (kulia) wataonesha makali leo?

LIGI kuu soka Tanzania bara raundi ya 12 inaendelea leo kwa mechi moja kupigwa uwanja wa Jamhuri Mkoani Morogoro kati ya wenyeji Polisi Morogoro na Yanga.

Hii ni mechi ya tatu ya ligi kuu kwa kocha wa Yanga, Hans van der Pluijm tangu arejee kuifundisha klabu hii akirithi mikoba ya Marcio Maximo.

Katika mechi mbili za kwanza, Pluijm hajapata ushindi kwani alitoka sare ya 2-2 na Azam fc na mchezo uliopita alivuna pointi moja pia kufuatia suluhu pacha ya bila kufungana dhidi ya Ruvu Shootings. Mechi zote zilipigwa uwanja wa Taifa Dar es salaam.

Kikosi cha Yanga kinachoaminika kuwa na washambuliaji wakali akiwemo Amissi Tambwe, Kpah Sherman, Saimon Msuva, Danny Mrwanda na Andrey Coutinho katika mechi tatu zilizopita kilikuwa butu katika umaliziaji wa pasi za mwisho na ikawalizimu baadhi ya wanachama kufikiria kuomba dua ya kutoa nuksi.

Ligi kuu iteandelea tena kesho jumapili kati ya Azam na Simba (Uwanja wa Taifa), Kagera Sugar na Ndanda (Uwanja wa CCM Kirumba), Stand United na Coastal Union (Uwanja wa Kambarage),, Mbeya City na Tanzania Prisons (Uwanja wa Sokoine), Ruvu Shooting na Mtibwa Sugar (uwanja wa Mabatini), na JKT Ruvu na Mgambo Shooting (Uwanja wa Azam Complex).



0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video