Okwi (kushoto) akiwa na Coordinator wa Simba, Salim Swaka muda huu uwanja wa Amaan
MSHAMBULIAJI hatari wa Simba, Mganda Emmanuel
Anord Okwi ametua leo mjini Zanzibar kujiunga na kambi ya klabu yake.
Okwi alikuwepo kwenye mechi ya desemba 26 mwaka huu Uwanja wa Taifa Simba ikipigwa 1-0 na Kagera Sugar, lakini aliondoka kwenda kumalizia fungate yake kufautia siku za karibuni kuoa mke.
Hivi tunavyozungumza, Okwi yupo hapa uwanja wa
Amaan akiwaangalia wachezaji wenzake wakiipashia Polisi kuelekea mchezo wa nusu
fainali ya pili ya kombe la Mapinduzi unaotarajia kuanza majira ya sa 2:15
usiku huu.
0 comments:
Post a Comment