MSHAMBULIAJI hatari wa Simba, Mganda Emmanuel Okwi
amefurahia kutwaa ubingwa wa kombe la Mapinduzi na kudai kuwa nguvu hiyo
wanaipeleka katika mechi za ligi kuu Tanzania bara.
“Kwanza ni jambo la furaha kutwaa ubingwa huu.
Nawashukuru sana wachezaji wenzangu”
“ Nimefurahi kurejea katika timu baada ya
mapumziko na hatimaye kutwaa ubingwa huu. Tutafanya vizuri ligi kuu, tunawaomba
mashabiki watuunge mkono”. Alisema Okwi.
Okwi aliongeza kuwa mbele yake anaona deni kubwa
kwa Wanasimba, hivyo anajitahidi kufanya mazoezi ya nguvu ili kurudi katika
hali yake.
“Kikubwa nafanya mazoezi kwa kujituma kwa lengo la
kufanya vizuri”. Aliongeza Okwi.
0 comments:
Post a Comment