Sunday, January 18, 2015

DSC_0116
MCHEZO wa ligi kuu ya soka Tanzania  Bara kati ya Mbeya City Fc na Kagera Sugar uliopigwa kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza jana umemalizika kwa City kuibuka na ushindi wa bao 1-0, lililofungwa na Peter Mapunda  katika dakika ya 80.

Mara baada ya mchezo huo kocha wa City  Juma Mwambusi aliwashukuru vijana wake kwa kucheza vizuri huku pia akiwapongeza kwa kuiwezesha timu yao kupata ushindi wa pili mfululizo.


“Tumecheza vizuri, nawapongeza waachezaji kwa kucheza kwa kiwango kizuri, hakika wamefanyia kazi yale yote tuliyowaeleza, huu ni ushindi wa pili mfululizo kwetu, sasa tunarudi nyumbani kujiandaa na mchezo unaofuata dhidi ya Prisons, shukurani zangu pia kwa mashabiki wetu ambao wamesafiri umbali mrefu kutoka Mbeya kuja kuisapoti timu yao hapa Mwanza “alisema Mwambusi akiongea na Tovuti ya klabu hiyo.
Katika mchezo huo ambao City ilicheza ikiwa na kumbukumbu ya ushindi wa bao 1-0 iliyoupata kwenye mchezo wa mzunguko wa 8 dhidi ya Ndanda Fc uliochezwa kwenye uwanja wa Sokoine jijini Mbeya wiki mbili zilizopita, ilianza kwa mashambulizi ya nguvu ambapo Themi Felix nusura aipatie bao la kuongoza mapema dakika ya 5 baada ya kupiga mpira uliogonga mwamba wa juu na kuokolewa na walinzi wa Kagera Sugar.

Ikicheza kwa pasi fupi na zenye kuonana City ilifanya shambulizi jingine kwenye lango la Kagera Sugar kwenye dakika ya 15 lakini shuti la Fredy Cosmas lilishindwa kulenga lango na mpira kutoka nje, Kagera walijibu shambulizi dakika ya 19  na kupata kona ambayo haikuweza kuzaa matunda hivyo hadi kipindi cha kwanza kinamalizika timu zote zilikuwa hazijafungana.

Mabadiliko aliyoyafanya Kocha Juma Mwambusi katika dakika ya 75 kwa kumtoa Cosmas Fredy na kumuingiza Peter Mapunda  yalikuwa na manufaa makubwa kwa City kwani dakika tano baadae Mapunda aliandika bao hilo  baada ya kuvisha kanzu golikipa wa kagera Sugar aliyetoka golini kujaribu kuwahi mpira uliokuwa umepigwa na Paul Nonga.

katika kipindi hicho cha pili Kagera Sugar walijitahidi kucheza kwa pasi fupi fupi na za haraaka kujaribu kurudisha bao hilo lakini uimara wa safu ya kiungo ya City iliyokuwa ikiongozwa na Stive Mazanda na pia Rafael Daud ilitosha kabisa  kuvuruga mbinu zote walikuwa wakizipanga  huku  uimara wa walinzi wa kati  Juma Nyoso na  Yusuf Abdalah ulikuwa makini kusafisha hatari zote , hivyo hadi mwisho  matokeo yalisomeka 1-0.


0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video