Friday, January 30, 2015

KUTOKANA na mwenendo mbovu wa Simba SC katika mechi za ligi kuu Tanzania bara, mchezaji wa zamani wa timu hiyo na kiongozi wa TFF, Mtemi Ramadhani amefanya mahojiano maalumu na mtandao huu na kuweka wazi sababu za Mnyama kuzidi kuboronga.

Mwandishi: Mtemi Ramadhani, wewe ni mchezaji wa zamani wa Simba, sasa hivi kumekuwa na malalamiko mengi ya wanachama na wapenzi wa Simba kuhusu mwenendo wa timu yao, kwa uzoefu wako wa kuwa kwenye mpira kwa miaka mingi unafikiri nini kinawasibu Simba saha hivi?


Mtemi: Suala la Simba liko wazi, mwenye kujua mpira anajua kwasababu mpira hauchezwi vyumbani, mpira unachezwa hadharani. Timu ilivyocheza Zanzibar kila mtu aliona, timu inavyocheza hapa kila mtu anaona, tatizo la Simba ni kwamba vijana wa Simba hawataki mazoezi.

Timu ya Simba haina mazoezi magumu, suala lao ni kwamba hawataki mazoezi. Simba wamecheza mechi sita kule Zanzibar, zilikuwa za mfululizo na walikuwa kambini, lakini baada ya pale walirudi kucheza na Ndanda. Nasikia tena wakafanya kambi siku moja kabla ya mpira, huwezi kucheza mpira bila kufanya mazoezi magumu hata siku moja, haiwezekani.

Simba hawajajiandaa vya kutosha, Simba ikicheza na timu yoyote inayofanya mazoezi magumu, ya kukimbia huku na kule, haiwezi kushinda kwa pumzi ile.

Na jambo zuri zaidi ni kwamba mipira inaonekana kwenye ligi nzuri, kama ni Afcon, kama ni Barcelona, Real Madrid,  wanaona duniani kote ambavyo mpira umebadilika, watu wanacheza kwa nguvu, wanakimbia, wanakaba. Simba mpaka mchezaji apate mpira ndio beki anakwenda kukaba, kwahiyo anatoa pasi kwa mwingine ambaye hajakabwa.

Simba hawezi kucheza mpira wa namna hiyo, hata iweje, na wanaweza kushuka daraja hivi hivi, si jambo la kuamini, lakini si la ajabu.


Mwandishi: Lawama kubwa zinatupiwa kwa uongozi, unafikri utawala nao unachangia mwenendo mbaya wa timu?


Mtemi: Naweza nikasema ndiyo! Ingawa si kwa asilimia kubwa. Lakini wanapaswa kusimamia timu, hawa walimu wa kizungu wana tatizo moja, tulikuwa na mzee mmoja alikuwa anaitwa Jan Poulsen pale TFF, timu ikifanya mazoezi asubuhi jioni anasema walale, ukimwabia tufanye hiki, anasema siku mbili wapumzike.

Binafsi niliwahi kuongea na mwalimu yule, akasema unajua mpira wa siku hizi hautaki mbio sana, si unao Barcelona wanavyocheza. Sasa ni jukumu la viongozi kusimamia, mwalimu anaweza kutoka na mambo yake ya ulaya, kamati ya utendaji inatakiwa imuite na kumwambia, “Bwana wachezaji wa Kiswahili wako moja, mbili, tatu na bila kufanya moja, mbili, tatu,hatuwezi kwenda”.

Sasa unamwachia mwalimu wa Kizungu ambaye anakuja na falsafa ya watu wa nje ambako wachezaji wanajitambua, wanalala majumbani kwao, wana mapesa mengi, mtu anatambua wajibu wake.


Hawa wa kwetu sio siri hawajitambui, tunawaona, mtu anatoka mazoezini  na gari yake ndani ana mwanamke, mwingine utasikia nusura apigwe chupa Kinondoni kwasababu ya kugombania mwanamke, hao ni wachezaji wa Simba, huwezi kucheza mpira namna hiyo.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video