VINARA wa ligi kuu soka Tanzania bara, Mtibwa
Sugar FC leo wametoka sare ya kufungana bao 1-1 na JKU ya Zanzibar katika
muendelezo wa michuano ya kombe la Mapinduzi linaloendelea kushika kasi uwanja
wa Amaan Zanzibar.
Mtibwa Sugar walikuwa wa kwanza kuandika bao la
kuongoza katika dakika ya 20 kupitia kwa mshambuliaji wa zamani wa JKT Ruvu,
Simba na DC Motemapembe ya DR Congo, Musa Hassan Mgosi.
Katika dakika ya 53, Mtibwa chini ya kocha Mecky
Mexime walipata mkwaju wa penalty baada ya beki wa JKU Hamis Abdallah kuunawa mpira
katika eneo la hatari, lakisi Mgosi akapewa alikosa tuta hilo kufuatia kupiga shuti
lililopaa juu ya lango, watoto wa mjini wanaita mnazi.
JKT walisawazisha bao hilo katika dakika ya 72
kupitia kwa Amour Omar.
0 comments:
Post a Comment