Tuesday, January 13, 2015

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar

MTIBWA SUGAR wamejiamini kuwafunga Simba katika mechi ya fainali ya kombe la Mapinduzi itakayopigwa leo majira ya saa 2:15 usiku uwanja wa Amaan Zanzibar.
Baada ya mazoezi ya jana asubuhi katika uwanja wa Mao Dse Tung mjini Zanzibar, Mtibwa walipumzika kutwa nzima na jioni hawakufanya mazoezi kabisa wakidai wamemaliza kazi.

“Hatuwezi kufanya mazoezi mara mbili kwa siku kwasababu ya Simba, tumefanya mazoezi asubuhi Mao Dse Tung, tumepumzika, tunawasuburi Simba kesho (leo). Tuko vizuri kwa kila kitu, waleteni”. Alisema msemaji wa klabu hiyo, Tobias Kifaru.


Mtibwa Sugar FC inayonolewa na nahodha wake wa zamani na Taifa Stars, Mecky Mexime , imewahi kutinga mara tatu katika hatua ya fainali ya michuano hiyo tangu ianzishwe 2007 ikifungwa na Yanga SC (2007), ikapoteza dhidi ya Simba SC (2008) kabla ya kutwaa taji lake la kwanza 2010 ilipoifunga Ocean View.

Timu hiyo ya Manungu, Turiani takriban km 100 kutoka mjini Morogoro, itaingia uwanjani leo ikiwa na nia ya kulipa kisasi kwa kufungwa na Simba SC katika fainali ya pili ya michuano hiyo 2008.

Mtibwa Sugar FC inaingia uwanjani pia ikihitaji kulinda heshima yake ya kutopoteza mechi hata moja ya mashindano msimu huu.Timu hiyo imecheza mechi 8 za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) msimu huu ikishinda nne (2-0 dhidi ya Yanga SC, 3-1 dhidi ya Ndanda FC, 1-0 dhidi ya Mgambo Shooting na 2-0 dhidi ya Mbeya City) na kutoka sare nne (0-0 Polisi, 1-1 Simba SC, 1-1 Kagera Sugar FC na 1-1 Stand United).

Aidha, Mtibwa Sugar FC haijapoteza hata mechi moja katika mechi zote tano zilizopita za Kombe la Mapinduzi mwaka huu, tatu za Kundi C ilizoshinda 1-0 dhidi ya Simba na kutoka suluhu na Mafunzo FC na sare ya 1-1 na JKU FC. Ikashinda kwa penalti 7-6 baada ya kutoka sare ya 1-1 na Azam FC robo-fainali kabla ya kuiondoa JKU kwa penalti 4-3 baada ya suluhu katika dakika 90 nusu-fainali jana.
???????????????????????????????
Wachezaji wa Simba wakishangilia moja ya goli walilofunga mechi za nyuma kombe la Mapinduzi

Mtibwa Sugar FC iliifunga Simba SC mabao 4-2 katika mechi yao iliyopita ya kirafiki kwenye Uwanja wa Azam, mechi iliyokuwa maalum kujipima nguvu kabla ya kuikabili Yanga SC katika mechi ya Nani Mtani Jembe 2.

Kwa kifupi, Simba SC haijawahi kuifunga Mtibwa Sugar FC nje ya Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam tangu kufariki kwa kiungo Mkongo Patrick Mafisango miaka mitatu iliyopita.

Kwa upande wao, wekundu wa Msimbazi, Simba SC, wamewahi kutinga fainali za Kombe la Mapinduzi mara nne wakiifunga Mtibwa Sugar FC 2008, wakaifunga Yanga SC 2011 kabla ya kufungwa na Azam FC 2012 na mwaka jana kufungwa na KCCA ya Ligi Kuu ya Uganda.

Simba SC wataingia uwanjani kesho wakisaka taji na pia kulipa kisasi cha kugeuzwa vibonde wa Mtibwa Sugar FC katika miaka mitatu iliyopita wanapocheza nje ya Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video