Sunday, January 25, 2015


Na Bertha Lumala, Morogoro

Mshambuliaji Danny Mrwanda wa Yanga SC ameanza kuhesabu katika timu yake hiyo mpya baada ya kuifungia bao katika ushindi wa 1-0 dhidi ya Polisi Moro katika mechi pekee ya leo ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) Uwanja wa Jamhuri mjini hapa jana jioni.

Mrwanda ameifunga timu yake ya zamani, Polisi Moro dakika ya 42 akimalizia mpira uliotemwa na kipa Tony Kavishe wa Polisi Moro kufuatia shuti kali la krosi ya beki wa pembeni kulia Juma Abdul wa Yanga SC.

Hilo ni bao la tano kwa Mrwanda baada ya kufunga pia mabao manne katika mechi saba alizokichezea kikosi cha Kocha Adolf Richard cha Polisi Moro mwanzoni mwa msimu huu kabla ya kujiunga na Yanga SC dirisha dogo.

Mrwanda, ambaye hakufunga katika mechi mbili zilizopita ambapo Yanga SC ilitoka sare ya 2-2 dhidi ya Azam FC na 0-0 dhidi ya Ruvu Shooting, sasa yuko sawa na Ame Ally Amour wa Mtibwa Sugar FC na Rashid Mandawa wa Kagera Sugar wenye mabao matano pia.

Mrwanda pia hakufunga bao hata moja katika mechi nne za Kombe la Mapinduzi visiwani Zanzibar mapema Januari mwaka huu, sawa na mshambuliaji mpya mwenzake kwenye kikosi cha Jangwani Mrundi Amisi Tambwe ambaye pia aliambulia kapa Zanzibar.

Mliberia Kpah Sherman alifunga mabao mawili Zanzibar ingawa hajaonesha cheche za mabao VPL. Tambwe, ambaye leo alikuwa benchi muda wote wa mechi, ameifungia Yanga SC bao moja katika mechi tatu za VPL zilizopita tangu ajiunge nayo dirisha dogo baada ya kutemwa Simba SC.
Kwa ushindi huo, Yanga SC ambayo imeshinda mechi nyingine nne msimu huu dhidi ya Tanzania Prisons, JKT Ruvu, Stand United na Mgambo ikishikwa kwa sare na Simba SC, Azam FC na Ruvu Shooting Stars na kufungwa na wakatamiwa Mtibwa Sugar FC na Kagera Sugar FC, imefikisha pointi 18 baada ya kucheza mechi 10.

Kikosi hicho cha Pluijm sasa kiko kimepanda hadi nafasi ya pili ya msimamo wa VPL kikizidiwa pointi mbili na vinara Azam FC ambao pia wamecheza mechi 10 na leo wanakipiga dhidi ya Simba SC Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

WAKALI WA KUCHEKA NA NYAVU
7. Didier Kavumbagu   Azam FC             
------------------------------------------------------------------
5. Ame Ally Amour      Mtibwa Sugar  
Rashid Mandawa         Kagera Sugar     
Danny Mrwanda         Polisi/Yanga SC  
-----------------------------------------------------------------
4. Rama Salim               Coastal Union    
Simon Msuva                Yanga SC             
Samwel Kamuntu        JKT Ruvu Stars   
------------------------------------------------------------------
3. Ally Shomary Sharif  Mtibwa Sugar    
Emmanuel Okwi          Simba SC            
-----------------------------------------------------------------
2. Aggrey Morris          Azam FC             
Amisi Tambwe             Simba/Yanga SC
Deus Kaseke                 Mbeya City FC
Ibrahim Hassan            Tanzania Prisons 
Jabir Aziz                      JKT Ruvu Stars
Jacob Masawe             Ndanda FC
Mussa Mgosi                Mtibwa Sugar FC
Najim Magulu              JKT Ruvu Stars 
Nassoro Kapama         Ndanda FC
Nicholas Kabipe          Polisi Moro 
Shaban Kisiga             Simba SC  

---------------------------------------------------------

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video