KOCHA wa Real Sociedad, David Moyes
ameisifu ngome yake ya ulinzi baada ya kuibuka na ushindi wa goli 1-0 dhidi ya
Barcelona jana jumapili.
Moyes alikuwa na furaha kidogo mwaka
jana, lakini amekuwa na furaha kubwa baada ya timu yake kuichapa Barca kufuatia
wao wenyewe kujifunga goli katika dakika ya pili kupitia kwa Jordi Alba.
Mscotish huyo alikuwa na msimu mgumu
Manchester United kabla ya kufukuzwa mwezi Aprili mwaka jana na kuamua kukubali
kazi ngumu ya kuifundisha Sociedad inayopambana kukwepa kushuka daraja tangu
mwezi novemba mwaka jana.
Kulikuwa na wasiwasi mkubwa katika
vyombo vya habari vya Hispania juu ya Moyes kukosa uzoefu wa soka la nchini
hiyo, kutojua lugha ya Kihispania, lakini ameanza kwa ugumu, ameimarisha timu
kuanzia beki na wamepoteza mechi moja tu mpaka sasa.
“Nina furaha sana kupata matokeo,
ilikuwa mechi muhimu na ngumu,” Moyes aliwaambia waandishi wa habari.
“Tulifanya jitihada kubwa ya kulinda
na tulijilinda kwa sehemu kubwa ya mechi. Huwezi kushinda mechi kama hujilindi
vizuri. Kwa namna tulivyocheza katika safu ya ulinzi kumefanikisha kupata
ushindi huu”
0 comments:
Post a Comment