Friday, January 23, 2015

WEKUNDU wa Msimbazi Simba wako tayari kuivaa Azam fc katika mechi ya ligi kuu soka Tanzania bara itayopigwa uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam jumapili jioni, januari 25.
Afisa habari wa Simba, Humphrey Nyasio amesema kikosi kipo shwari na kocha anaendelea kukamilisha programu nzima ya mechi hiyo.

“Sisi tunaendelea vizuri, wachezaji wote wapo kambini kasoro waliokuwepo Taifa Stars Maboresho. Tunawarajia leo kuungana na wenzao na watafanya mazoezi ya pamoja”. Amesema Nyasio.

Aidha Nyasio ameweka sawa mkanganyiko uliopo miongoni mwa wadau wa soka wakidhani mechi itapigwa kesho januari 24 kama ilivyopangwa.


“Nashangaa watu wanatangaza mechi ipo kesho (jumamosi), mechi ni jumapili januari 25. Yalifanyika marekebisho ya ratiba kutokana na mechi ya jana ya Taifa Stars Maboresho dhidi ya Rwanda”. Ameongeza Nyasio.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video