MAISHA ni safari ndefu…katikati pitapita yangu nimemkuta
beki wa kushoto wa Mtibwa Sugar, David Charles Luhende akipumzika maeneo fulani
hivi.
Mwandishi: Luhende niaje mkali wangu?
Luhende: Barida mzazi, mishe vipi?
Mwandishi: Mbona kama unawaza hivi?
Luhende: Kiaina Babu! Si unajua maisha safari
ndefu.
Mwandishi: kwanini unasema hivyo?
Luhende: Ujue mie mpira bwana ni kazi yangu. Kabla
ya kuanza kucheza soka miaka ya nyuma kuna kazi nilikuwa nafanya, daah! Acha tu
rafiki yangu.
Mwandishi: Kazi gani hiyo?
Luhende: Mimi ni fundi mekanika kaka, nimetengeneza
sana magari huko nyuma. Nakumbuka nilikuwa Napata 300, 400 na nikipata sana
500.
Mwandishi: Ulisomea ufundi mekanika?
Luhende: Hapana, ujanja ujanja tu! Tena baba
alikuwa anapenda nifanye kazi hii kuliko hata mpira. Sema mama alipenda sana
nicheze mpira.
Hata saizi mtu kama ana tatizo na gari lake aje
nifanye kazi,lakini lazima anitoe..hahahahahah!
Mwandishi: umetisha sana kijana, sema tutaonana
mida tupige stori vizuri!
Luhende: Poa jomba…unafanya vizuri sana!
Mwandishi: Ahsante kijana wa Mecky Mexime.
0 comments:
Post a Comment