ORODHA ya mwisho ya wachezaji watatu wanaowania
tuzo ya mwanasoka bora wa dunia FIFA Ballon d'Or inayofanyika leo jumatatu
mjini Zurich, Uswizi, wametangazwa ambao ni Lionel Messi, Manuel Neuer na
Cristiano Ronaldo.
Hizi ni takwimu zinazowafanya Ronaldo na Messi
waingie katika kinya’anyiro cha mwisho kwa mwaka 2014.
Messi: Baada ya kufunga goli moja katika fainali
za kombe la dunia zilizopita (2010), Lionel Messi alifunga mabao manne katika
fainali za mwaka 2014 na kushinda kiatu cha mchezaji bora wa mashindano.
Alikuwa na magoli 52 katika mechi 62 za klabu na nchi yake, pia akiongeza ya La
Liga na UEFA aliyofunga mwezi uliopita.
Cristiano Ronaldo: Alishinda tuzo iliyopita ya Ballon
d'Or, alifunga magoli 69 katika mechi 59 za Real Madrid na Ureno mwaka 2013. Akiwa
na mabao 55 katika mechi 55 mwaka huu ni rekodi kali, ingawa mabao yake 45
katika ligi na mashindano ya ulaya ni magoli sita zaidi ya mchezaji yeyote
aliyefunga katika michuano ya mwaka huu katika ligi tano za juu. Pia aliweka
rekodi ya kufunga magoli mengi zaidi katika msimu mmoja wa UEFA, akifunga
magoli 17 katika msimu wa 2013-14.
0 comments:
Post a Comment