Tuesday, January 20, 2015

MBEYA CITY FC imetoka sare ya kufungana goli 1-1 na CDA ya Dodoma katika mechi ya kirafiki iliyopigwa jana uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma.

Mechi hiyo ilitumika na kocha Juma Mwabusi kama sehemu ya kuangalia makosa katika kikosi chake kabla ya kuivaa Tanzania Prisons wikiendi hii uwanja wa Sokoine Mbeya.

City na Prisons ni mahasimu wa jiji la Mbeya na kila wanapokutana cheche zinawaka moto uwanjani.

Timu zote zitaingia katika mchezo huo wa jumamosi zikiwa na kumbukumbu tofauti.


Mwishoni mwa wiki iliyopita, City waliifunga Kagera Sugar bao 1-0 uwanja wa CCM Kirumba, wakati Prisons walitoka 0-0 na Mgambo JKT uwanja wa CCM Mkwakwani Tanga.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video