WAGONGA nyundo wa Mbeya, Mbeya City fc wapo tayari
kwa mechi ya kesho ya ligi kuu soka Tanzania bara dhidi ya Kagera Sugar
itakayopigwa uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Timu zote mbili zitakuwa ugenini ‘neutral ground’
kitendo kilichofurahiwa na Mbeya City fc.
“Tungekuwa Kaitaba kungekuwa na presha kubwa. Ujue
uwanja wa Kirumba hauna mwenyeji kesho, wote kama vile tuko ugenini, tutaonesha
kandanda safi na kuvuna pointi tatu”. Alisema Afisa habari wa Mbeya City ,
Dismas Ten alipohojiwa na mtandao huu kutoka Mwanza.
0 comments:
Post a Comment