Monday, January 19, 2015

DSC_0026
WAGONGA Nyundo wa Mbeya, Mbeya City fc leo jioni wanakabiliana na CDA ya Dodoma katika mechi ya kirafiki itayofanyika uwanja wa Jamhuri Mkoani Dodoma.

Afisa habari wa Mbeya City, Dismas Ten ameuambia mtandao huu kuwa mechi hiyo ambayo ni sehemu ya maandalizi ya mechi ya wikiendi dhidi ya mahasimu wao wa jiji, Tanzania Prisons itatumiwa na kocha Juma Mwambusi kuongeza makali ya wachezaji wake.

 Kwa upande wa kocha mkuu Juma Mwambusi amekaririwa na Tovuti ya klabu hiyo leo akisema:  “Tumetoka kushinda mchezo uliopita  kwenye uwanja wa ccm kirumba na jumamosi ijayo tutakuwa na  mchezo mwingine huko Mbeya dhidi ya Tanzania Prisons, tuko hapa Dodoma kwa maandalizi ya mchezo huo ingawa kwetu sisi kucheza na CDA ni sehemu ya kudumisha udugu wetu kimichezo, binafsi  nina imani kubwa na timu yangu na kwa uwezo wa mwenyezi mungu naamini  tutashinda pia  mchezo ujao  wa ligi kwa sababu tunataka kupata pointi tatu kwenye kila mchezo unaokuja mbele yetu”. Amesema Mwambusi.

Katika hatua nyingine Afisa masoko wa City Joseph Semu amesema kuwa jezi za msimu huu  zitakuwepo uwanjani hivyo mashabiki wote wenye kiu ya kuvaa jezi hizo waje uwanjani na zitauzwa hapo kwa bei nzuri kabisa.


Mbeya City ilianza vibaya ligi, lakini safari hii imepata ushindi mara mbili mfululizo kwani kabla ya kuifunga Kagera, iliitandika Ndanda fc bao 1-0 katika mechi ya ligi kuu iliyopigwa desemba 28 mwaka jana. 

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video