WAGONGA Nyundo wa Mbeya, Mbeya City fc wamesema
hawana homa yoyote kuelekea mechi ya watani wa jiji, ‘Mbeya Derby’ dhidi ya Tanzania Prisons ‘Wajelajela’
itayopigwa jumapili januari 25 mwaka huu uwanja wa CCM Sokoine Mbeya.
Afisa habari wa klabu hiyo, Dismas Ten
ameuthibitishia mtandao huu kuwa kikosi cha Mbeya City kipo salama, wachezaji
wapo katika morali ya hali ya juu kuhakikisha wanavuna ushindi wa tatu
mfululizo.
“Sisi hatuna homa yoyote, mara ngingi tunapokutana
na Prisons, historia inatubeba, tumejiandaa na tunaamini tutachukua pointi tatu
muhimu”. Amesema Dismas na kuongeza. “Baada
ya ushindi dhidi ya Ndanda na Kagera Sugar, Mwalimu Mwambusi amekuwa na kazi ya
kuendeleza mafanikio hayo, amekiandaa kikosi vizuri na bila shaka tutafanya
vizuri”
Mbeya City kwa sasa wapo nafasi ya 9
wakijikusanyia pointi 11 nyuma ya Ruvu Shootings wenye pointi 12, ingawa wao
wamecheza mechi 11 wakati Wanazambarao wameshuka dimbani mara 9.
City imeshinda mechi tatu, imepoteza mechi nne na
kutoa sare mechi mbili.
0 comments:
Post a Comment