Manyika
Peter akijifua na timu yake ya Simba katika Uwanja wa Amaan Zanzibar walipokuwa
wakishiriki michuano ya Kombe la Mapinduzi.
Goli kipa namba mbili wa klabu ya
Simba Manyika Peter, leo amechagulia na Kocha mkuu wa timu ya Taifa Mart Nooij
kujiunga na Timu ya Taifa ya Maboresho ambayo inakabiliwa na mchezo wa kirafiki
na Rwanda hapo January 22 mwaka huu ikiwa ni kwa mara ya kwanza.
Mbali na Manyika pia Kiungo
chipukizi wa Yanga Salum Telela amejumuishwa katika kikosi hicho kwa mara ya
kwanza baada ya kuonyesha kiwango cha juu akiwa na Klabu yake hiyo ya Jangwani.
Nooij amesema kuwa Stars wataingia
kambini januari 18, ambapo wachezaji 16 watakuwa kambi ya Dar es salaam na
wengine 10 wataingia kambi ya Mwanza, itakapo fika januari 19, Wachezaji wote
wa Dar es salaam na Mwanza wataungana kambini sehemu moja jijini Mwanza tayari
kwa mechi januari 22 ndani ya Uwanja wa CCM Kirumba.
Wachezaji wengine ni Aishi Manula
kutoka Azam FC, Benedict Tinoco wa Kagera Sugar na Manyika Peter wote ni
makipa.
Mabeki ni Miraji Adam wa Mtibwa
Sugar, Andrew Vicent wa Mtibwa Sugar, Gadiel Michael Mbaga wa Azam FC, Emanuel
Semwanda wa African Lion, Joram Mgeveke wa Mwadui, Edward Cherles wa Yanga,
Mohamed Hussein wa Simba na Salum Mbonde wa Mtibwa Sugar.
Viungo ni Salum Telela wa Yanga,
Adam Paulo Salamba wa Bulyankulu SC, Hassan Banda wa Simba, Said Juma Makapu wa
Yanga, Said Hamis Ndemla wa Simba, Hassan Dilunga wa Yanga, Hussein Moshi
Malombe wa Geita Gold SC, Shiza Ramadhani wa Mtibwa Sugar, Omary Nyenje wa
Ndanda FC, pamoja na Alfred Juma Masumbakenda wa Bulyankuru
Source: hivisasa.co.tz
0 comments:
Post a Comment