Simba wakifanya mazoezi walipokuwa Zanzibar
KIKOSI cha Simba SC leo jioni kimefanya mazoezi
Uwanja wa CCM Nangwanda Sijaona mkoani Mtwara kujiandaa na mechi ya keshokutwa
ya ligi kuu soka Tanzania katika uwanja huo dhidi ya wenyeji Ndanda fc ‘Mtwara
Kuchele’.
Afisa habari wa Simba, Humphrey Nyasio amesema
wachezaji wote wapo salama na kocha Goran Kopunovic ana matumaini makubwa ya
kuchukua pointi tatu muhimu.
“Tumefanya mazoezi leo jioni, kocha amewaona
wachezaji wake na akasema wapo fiti. Ndanda lazima wana hofu, wameona mambo
makubwa tuliyofanya kombe la Mapinduzi”.
Simba walifanikiwa kutwaa ubingwa wa kombe la
Mapinduzi 2015 kufuatia kuifunga Mtibwa Sugar penalti 4-3 katika mechi ya
fainali iliyopigwa januari 13 mwaka huu.
0 comments:
Post a Comment