MABINGWA watetezi wa kombe la Mapinduzi, KCCA Ya Uganda
wameibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Mtende ya Zanzibar katika mchezo uliomalizia
dakika chache zilizopita uwanja wa Amaan Zanzibar.
Mabao ya KCC katika mchezo yamefungwa na Waswa
Herman katika dakika ya 40, na Wadri William katika dakika ya 65 na 66.
Mechi ianayoanza hivi punde ni baina ya Yanga
dhidi ya Polisi.
Katika mechi nyingine iliyopigwa uwanja wa Mao Dse Tung, Taifa ya Jang'ombe imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Shaba, zote za Zanzibar.
Katika mechi nyingine iliyopigwa uwanja wa Mao Dse Tung, Taifa ya Jang'ombe imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Shaba, zote za Zanzibar.
0 comments:
Post a Comment