Wednesday, January 28, 2015




Kiungo mshambuliaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid, Barcelona na timu ya taifa ya Ureno Luis Figo  ametangaza rasmi uwamuzi wake wa kugombea Urais katika shirikisho la mpira wa miguu duniani Fifa mwaka huu lengo kubwa ni kumng’oa Rais aliyepo madarakani kwa sasa Sepp Blatter.


Mwisho wa wagombea kutangaza kugombea nafasi hiyo ni alhamisi wiki hii, lakini Figo ameamua kutangaza mapema akiwa na wapambe watano wanaomsapoti kutoka Fifa.


Figo alisema anaupenda sana mpira wa miguu, ni wakati sahihi sasa kufanya marekebisho katika shirikisho la mpira wa miguu duniani Fifa kwani shirikisho hilo limekuwa na picha mbaya baada ya kutotekeleza mambo muhimu katika mchezo wa soka.

"Naupenda sana mpira wa miguu nisingependa kuona unadidimizwa na watu wasiopenda maendeleo yake, lakini pia kuirudisha picha nzuri ya shirikisho ambayo imeharibiwa na viongozi ambao wapo madarakani kwa sasa, ndio maana nimeamua kugombea nafasi ya Urais katika shirikisho,’’ Figo aliliambia shirika la utangazi CNN.

"nimekuwa nikuzungumza na watu wengi sana ambao ni muhimu katika mchezo wa soka kama vile wachezaji, makocha pamoja na marais wa mashirikisho mbalimbali ya mpira na wote wanafikiria kama mimi kwamba lazima kuwe na mabadiliko,”aliongeza Luis Figo

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video