Liverpool wanaitaka saini ya mshambuliaji wa Burnley, Danny Ings
BOSI wa Liverpool, Brendan Rodgers anajitabiria kufanya vizuri kufuatia kurejea kwa mshambuliaji wake Daniel Sturridge.
Wakati huo huo Wekundu hao wa Anfiedl wanaiwania saini ya mshambulizi wa Burnley, Danny Ings.
Mshambuliaji huyo wa England, Sturridge ameimarika kiafya kufuatia kukaa nje ya uwanja kwa muda mrefu akisumbuliwa na majeruhi na kesho atapangwa kwenye kikosi kitakachoivaa West Ham kwenye mechi ya EPL.
Rodgers amekosa mshambuliaji msumbufu kwa mabeki, lakini uwepo wa Sturridge utawafanya wawe na makali na sasa wanaangalia uwezekano wa kumsajili Ings wa Burnley katika dirisha dogo la usajili.
0 comments:
Post a Comment