Frank Lampard akizuiwa na Atdhe Nuhiu wa Sheffield katika mechi ya raundi ya tatu ya kombe la FA
FRANK Lampard anatarajia kuondoka Manchester City mwishoni mwa msimu huu na kujiunga na klabu yake ya New York City mwezi Julai mwaka huu.
Licha ya kiwango cha juu anachoonesha Lampard chini ya Manuel Pellegrini, kiungo huyo ameweka wazi kuwa anahitaji kupata changamoto ya kucheza ligi ya Marekani (MLS) pale mkataba wake wa mkopo utakapomalizika nchini England.
Kumekuwepo na wasiwasi katika klabu ya New York City na ligi ya MLS kwamba Lampard mwenye miaka 36 anaweza kushawishika kubakia Etihad hata baada ya msimu kumalizika.
0 comments:
Post a Comment