AFISA habari wa Ruvu Shootings mwenye
maneno mengi kama njugu, Masau Bwire amehudhuria mechi ya Polisi Morogoro dhidi
ya Yanga inayochezwa jioni ya leo uwanja wa Jamhuri Mkoani Morogoro.
Akiwa mjini humo Masau ameandika
katika kundi maarufu la ‘Kijiwe cha soka’ lilipo katika mtandao wa kijamii wa facebook
akisema: “Nipo Moro. Kwa namna hali ilivyo,
nitakuwepo uwanjani lakini haitakuwa
rahisi ninyi
kuniona. Kwa uchunguzi nilioufanya
nikiwa hapa Moro, Yanga
wana asilimia kubwa
sana kushinda mechi ya leo!”
0 comments:
Post a Comment