Goran na Ivo Mapunda walikumbatiana kwa muda mrefu baada ya kutwaa ubingwa
KOCHA mkuu wa Simba, Mserbia Goran Kopunovic
amesema kipa wake Ivo Mapunda ni shujaa mkubwa na uzoefu wake unaisaidia timu.
Kopunovic aliuambia mtandao huu baada ya kipa huyo
kudaka penalti ya mwisho ya Vicent Barnabas wa Mtibwa na kuwapa Ubingwa Simba
kuwa aliamua kufanya mabadiliko ya kumtoa Peter Manyika ‘Junior’ na kumuingiza
Ivo kwasababu ya uzoefu.
“Ivo ni kipa mzoefu sana, ndio maana nilimuingiza,
angalia alichofanya, nimefurahi sana na imetupa morali kubwa”
Kocha huyo amewapongeza wachezaji wake kwa
kupigana mwanzo mpaka mwisho ingawa hawajakaa naye kwa muda mrefu.
“Tumechukua Mapinduzi, lakini malengo yetu ni ligi
kuu. Kweli mechi hii ilikuwa muhimu sana, ila ligi ni muhimu zaidi”. Alisema
Kopunovic.
0 comments:
Post a Comment