Mkude (kulia) akiwa kazini
KIUNGO mkabaji wa Simba, Jonas Gerrard Mkude
amesema kutwaa ubingwa wa kombe la Mapinduzi ni mwanzo mzuri wa kufanya vizuri
katika mechi za ligi kuu Tanzania bara.
Mkude ameuambia mtandao huu kuwa kocha Goran Kopumovic
amekuja na mbinu mpya ambazo zinawasaidia kuwa imara.
“Kocha anataka kushambulia kwa kasi na kukaba
sana. Ni mwalimu mzuri. Ujue kila mwalimu ana ubora wake. Hata Phiri (Patrick)
alikuwa mzuri, sema kuna kutofautiana”.
Kiungo huyo tegemeao alisema mafanikio ya ubingwa
wa Mapinduzi ni umoja na mshikamano kwa wachezaji wote wa Simba, mashabiki na
viongozi.
“Mechi haikuwa rahisi, lakini tulijituma kwa
dakika zote na hatimaye tumevuna matokeo mazuri”. Alisema Mkude.
0 comments:
Post a Comment