Wednesday, January 7, 2015

Mrisho Ngassa

KOCHA mkuu wa Yanga SC, Mholanzi, Johannes Hans van der Pluijm anaamini Mrisho Ngassa atarudi katika kiwango chake cha zamani.

Pluijm alikiri wazi kuwa nyota huyo ameshuka kiwango kwa sasa  na ndio maana anaanzia benchi katika mechi mbalimbali, lakini anaonesha juhudi kubwa mazoezini kitendo kinachoonesha wazi ametambua alipo sasa.

“Kiwango cha Ngassa kimeshuka, lakini ni mchezaji mwenye akili, lazima atarudi katika kiwango chake”. Alisema Pluijm.

Kocha huyo anayependa soka la kushambulia aliongeza kuwa kwasasa kikosi chake kimesheheni nyota wa kiwango cha juu, hivyo inawalazimu wachezaji kufanya jitihada za kumshawishi.

Moja kati ya mechi kubwa ambayo Ngassa hakuanza chini ya Pluijm mwishoni mwa mwaka jana ni ile ya ligi kuu soka Tanzania bara dhidi ya Azam fc iliyopigwa desemba 28 mwaka jana uwanja wa Taifa ambapo timu hizo zilitoka sare ya 2-2.

Katika mechi hiyo, Ngassa alichezeshwa dakika 7 tu kitendo kilishoashiria mchezaji huyo kipenzi kwa Wana Yanga si mchezaji tegemeo tena katika kikosi cha Yanga.

Kocha huyo aliongeza kuwa siku zote anapenda kucheza mpira wa wazi, akishambulia zaidi kwa lengo la kufunga magoli mengi, hivyo nguvu zake zipo katika kuwanoa viongo wake na washambuliaji wake.


Kwasasa Pulijm anapenda kuwatumia zaidi Kpah Sherman, Danny Mrwanda, Amissi Tambwe, Saimon Msuva, Andrey Coutinho katika safu ya ushambuliaji, huku Ngassa, Hussein Javu wakianzia benchi.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video