Friday, January 30, 2015

Steven Mazanda

KIUNGO mahiri wa Mbeya City fc, Steven Mazanda amesema wapo katika hali nzuri kuelekea mechi ya kesho ya ligi kuu Tanzania bara dhidi ya Polisi Morogoro itayopigwa uwanja wa Jamhuri Morogoro.

Mazanda ameuambia mtandao huu muda huu kwa njia ya simu kutoka mji kasoro bahari kuwa hawezi kuwaogopa Polisi.

“Mpira ni kazi yangu, nitawaogopaje Polisi?, tuko vizuri kwa ajili ya mechi”. Amesema Mazanda.

Kiungo huyo mwenye ufundi mwingi amesema wamepita wakati mgumu, lakini siri ya kurejesha makali ni kujituma na kukubali kukosea, halafu kujifunza upya.

Mazanda aliyekuwepo katika kikosi cha kwanza kilichoifunga Simba mabao 2-1 katikati ya wiki hii (januari 28 mwaka huu) amesema wapinzani hao waliochanganyikiwa na kipigo inabidi wakubali changamoto na kujipanga upya.


“Wavumilie, mpira ndivyo ulivyo. Hata sisi tulipita wakati wa mpito”. Amesema Mkongwe huyo aliyepachikwa jina la ‘Babu’.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video