KIJANA mpole ambaye hapendi makuu wala kuzungumzia
mambo ya mpira akiwa likizo, Hassan Suleiman Isihaka ameteuliwa kuwa nahodha wa timu ya Simba
akisaidiwa na Jonas Mkude.
Isihaka ambaye hupendelea zaidi mtandao wa kijamii
wa Watsup ‘kuchati’ na marafiki zake ameteuliwa jana na kocha mkuu wa klabu hiyo, Mserbia Goran
Kopunovic baada ya mazoezi ya muda mfupi uwanja wa Boko Veteran.
Hata hivyo kocha huyo ameteua wachezaji wakongwe
ambao watakuwa wanawashauri pale yanapohitajika maamuzi ya busara.
Wachezaji hao ni Ivo Mapunda, Shaaban Kisiga, Masoud
Nassor ‘Cholo’ na Mganda Emmanuel Okwi.
Isihaka alianza kuiongoza Simba katika michuano ya
kombe la Mapinduzi ambapo klabu hiyo ilitwaa ubingwa kwa kuifunga Mtibwa Sugar
Penalti 4-3 katika mechi ya fainali iliyopigwa januari 13.
0 comments:
Post a Comment