Wachezaji wa Simba, kutoka kulia, Jonas Mkude, Ramadhani Singano 'Messi', Elius Maguli, Said Ndemla na Danny Sserunkuma wakijiandaa kuanza mechi jana usiku
BEKI wa kulia wa Simba, Hassan Ramadhan Kessy
amewataka Wanasimba wote kuiunga mkono timu yao ili kufanya vizuri katika
michuano ya ligi kuu.
Kessy aliuambia mtandao huu jana usiku baada ya
Simba kushinda bao 1-0 dhidi ya JKU na kufuzu robo fainali ya kombe la
Mapinduzi kuwa;
‘Simba ni timu yetu wote. Umoja utatupatia
mafanikio. Niwaambie mashabiki wa Simba, hii ni timu yetu, tusitengane”.
Alisema Kessy.
Beki huyo anayepanda na kushambulia kupitia winga
ya kulia aliongeza kuwa kocha mpya amekuja, mbinu zake ni nzuri, kinachotakiwa
na kumpa muda ili atimize malengo ya timu.
Kessy aliyesajiliwa na Simba wakati wa dirisha
dogo mwezi desemba mwaka jana akitokea Mtibwa Sugar alikuwa na uhakika wa namba
katika kikosi cha Patrick Phiri.
Alicheza kwa mara ya kwanza katika mechi ya kirafiki dhidi ya Mwadui fc
uwanja wa Taifa Dar es salaam, akakipiga dhidi ya Taifa ya Jang’ombe uwanja wa
Amaan Zanzibar(mechi ya kirafiki) na akacheza mechi ya kwanza ya ligi kuu dhidi
ya Kagera Sugar, mechi iliyomfukuzisha kazi Phiri baada ya kulala kwa bao 1-0.
Katika michuano ya Mapinduzi inayoendelea visiwani
hapa, beki huyo amecheza mechi zote tatu , moja chini ya Seleman Matola dhidi
ya Mtibwa Sugar ambapo Mnyama alipigwa 1-0 na mechi mbili dhidi ya Mafunzo na
JKU chini ya Goran Kopunovic, Simba ikishinda zote kwa bao 1-0.
0 comments:
Post a Comment