Saturday, January 17, 2015


WAGONGA nyundo wa Mbeya, Mbeya City fc wameanza kurejesha makali yao baada ya kuitandika bao 1-0 Kagera Sugar katika mechi ya ligi kuu soka Tanzania bara iliyomalizika jioni hii uwanja wa CCM Kirumba Mwanza.

Bao hilo pekee limefungwa dakika ya 80 na Peter Mapunda.

Kikosi hicho cha Juma Mwambusi kilishangiliwa na zaidi ya mashabiki 200 waliosafiri kutoka Mbeya kuipa sapoti timu hiyo.

Ushindi wa huu ni wapili mfululizo kwani desemba 28 mwaka jana waliibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Ndanda fc katika mechi ya raundi ya nane ya ligi kuu kwenye uwanja wa Sokoine Mbeya.


Mbali na Kirumba, Uwanja wa CCM Mkwakwani Tanga ulikuwa na kibarua cha kuhimili daluga za maafane wawili, Mgambo JKT dhidi ya Tanzania Prisons katika mechi ya ligi kuu soka Tanzania bara iliyocheza jioni ya leo.


Mechi hiyo imemalizika kwa timu zote kutoka suluhu (0-0).

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video