Sunday, January 18, 2015

DSC_0023
NAHODHA wa Mbeya City fc Mwengane Yeya amesema kikosi cha nyota 11 waliokuwepo uwanjani kwenye mchezo wa ligu kuu ya Vodacom  dhidi ya Kagera Sugar uliochezwa uwanja wa CCM Kirumba-Mwanza  walicheza vizuri na kwa kiwango bora jambo lililochangia Mbeya City Fc kuibuka na ushindi wa bao 1-0.

Akizungumza na Tovuti rasmi ya klabu hiyo mara baada ya mchezo kumalizika jana jioni, Yeya aliyekuwa kwenye orodha ya wachezaji wa akiba alisema kuwa  nidhamu ya hali ya juu uliyooneshwa na wachezaji wote  waliokuwa uwanjani na waliokuwa kwenye bechi imesababisha kupatikana kwa ushindi huo kufuatia ushirikiano mkubwa uliouwepo.


“Hakika timu imecheza vizuri, kulikuwa na ushirikiano mkubwa kati yao, zaidi walikuwa na nidhamu ya hali ya juu ndiyo maana umeona kuna wakati mwamuzi alikuwa anatoa maamuzi ya utata lakini hawakuliangalia hilo walibaki mchezoni wakajituma muda wote nasi tuliokuwa benchi tuliwapa sapoti, hili limenifurahisha sana, tunashukuru kupata pointi tatu ugenini hii ni hamasa ya kupata tatu zingine kwenye mchezo unaofuata  ambao tutacheza nyumbani” Yeya amekaririwa na Tovuti ya klabu.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video