Monday, January 19, 2015

WAKATA miwa wa Kaitaba, Kagera Sugar FC wamesema sasa wameiva kuivaa Azam fc katika mchezo wa kiporo wa ligi kuu soka Tanzania bara utakaopigwa kesho (januari 20) uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.

Kocha msaidizi wa ‘Wanankurukumbi’ hao, Murage Kabange amesema baada ya kutandikwa bao 1-0 dhidi ya Mbeya City jumamosi iliyopita, hawatakubali kuacha pointi tatu kwa mara nyingine mbele ya mabingwa watetezi.

“Tumejipanga, tumezungumza na vijana, tumewajenga kiakili na muda wote asubuhi tumefanya mazoezi mepesi, tuna matumaini kwamba kesho tutfanya vizuri katika mchezo huo ambao utakuwa mgumu kwasababu wenzetu walikotoka wamepata matokeo, kwahiyo wamekuja na nguvu ya kupata pointi tatu ambazo ni muhimu kwao”. Amesema Kabange katika mahojiano na mtandao huu. Aliongeza. “Tulipoteza mechi, lakini si kweli kwamba ukipoteza mechi basi kunakuwa na matatizo, naweza kusema hatukuwa na bahati kwasababu sikuona nini ambacho wenzetu walituzidi zaidi ya nafasi ile moja waliyoipata na kufunga goli dakika ya 80”.

Wakati huo huo Azam fc wamefanya mazoezi asubuhi uwanja wa CCM Kirumba kuweka miili sawa kabla ya mechi ya kesho.

Meneja wa klabu hiyo, Jemedari Said Mzumari amesema wamekusudia kuchukua pointi sita kanda ya Ziwa na kumalizia za Simba Dar es salaam, kisha kwenda Lubumbashi,  DR Congo tayari kwa maandalizi ya ligi ya mabingwa.


Azam waliibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya wenyeji Stand United katika mechi ya ligi kuu iliyopigwa jumamosi uwanja wa CCM Kambarage, Shinyanga.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video